Na Grace Michael, Mwanza
MKUU wa Mkoa wa Mwanza, Evarist Mbigiro amezitaka Halmashauri mkoani humo kuzitumia fedha zinazolipwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika ununuzi wa dawa na si kuzielekeza katika masuala mengine kama ya kulipana posho.
Amesema kuwa fedha hizo zimekuwa zikitumika katika matumizi ambayo hayakukusudiwa jambo linalokwamisha uboreshaji wa huduma za matibabu katika vituo vya kutolea matibabu.
Agizo hilo amelitoa katika mkutano wa wadau wa Mfuko huo uliofanyika leo jijini Mwanza na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo watoa huduma, wanachama, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Wilaya na wengine.
"Wenzetu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wanatulipa fedha lakini fedha hizo ndo utazikuta zinalipwa posho huku vituo vikikosa dawa...hili halikubaliki ni lazima tuone fedha hizi zikinunua dawa na wananchi wakipata tiba na kuwa na afya njema," alisema Mbigiro.
Alisema kuwa yeye kama Mkuu wa Mkoa atajisikia faraja kuona akiongoza wananchi wenye afya njema kwa kuwa watakuwa na uhakika wa kuzalisha na kukuza pato lao na la Taifa kwa ujumla.
Alisema kuwa inashangaza Mkoa kama wa Mwanza kuwa nyuma katika suala la wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) huku ukiwa na fursa nyingi za kiuchumi na pato la mwananchi wa Mwanza likikidhi mahitaji ya kujiunga na Mfuko huo ili kuwa na uhakika wa matibabu.
"Hapa tuna fursa nyingi zikiwemo za uvuvi, ufagaji, kilimo, madini, utalii na zingine na ili hizi fursa zitumike ni lazima wananchi hawa wawe na afya njema hivyo ni lazima tuhakikishe sisi viongozi tunawahamasisha wananchi wetu kwa kuwaeleza umuhimu wa kuwa na bima ya afya...sitakubali mkoa huu kubaki na asilimia 1.1 ya kaya zilizoko kwenye Mfuko wa CHF," alisema.
Kutokana na hali hiyo, alisema kuwa Uongozi wa Mkoa wa Mwanza utatoa ushirikiano kwa NHIF ili lengo la kuwafikia Watanzania asilimia 30 ifikapo 2015 lifanikiwe.
Aliongeza kuwa hata Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2010 katika ibara ya 85 inasema wazi kuwa "Mandeleo ya Taifa letu yataletwa na wananchi wenye afya bora inayowezesha kuzalisha mali na kutoa huduma mbalimbali".
Mbigiro akitoa mwito kwa wanachama wa Mfuko huo, aliwataka kuwa walinzi wa huduma za Mfuko hasa wanapokutana na dawa zinazotolewa na Serikali zikiuzwa kwenye maduka binafsi.
Ili kutimiza lengo la kupanua wigo wa wanachama wa Mfuko huo, Mbigiro alizitaka Halmashauri kutunga sheria ndogo itakayowalazimu wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Emanuel Humba akitoa maelezo ya Mfuko huo kwa wadau, aliwataka watoa huduma kutumia fursa mbalimbali zinazotolewa na Mfuko huo ili kuboresha huduma za matibabu.
Aliahidi kuwa Mfuko utaendelea na juhudi za kutoa elimu kuanzia ngazi ya Taifa hadi ngazi ya kaya ili kuhakikisha lengo la afya bora kwa kila Mtanzania linafikiwa.
Tuesday, March 27, 2012
Tuesday, March 20, 2012
CHF italeta afya bora na kupunguza umasikini-Pinda
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda ameagiza Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) uwe agenda ya Kitaifa kwa kuwa ndio njia pekee ya kufikia lengo la Afya Bora kwa wote na kupunguza vifo na umasikini kwa Watanzania.
Kutokana na umuhimu huo, ameiagiza Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kukaa na Uongozi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ili kuandaa mkakati utakaohakikisha Watanzania wote wanapata huduma za Mfuko huo kwa lengo la kuwawezesha kuwa na afya njema.
Waziri Mkuu Pinda aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati wa maadhimisho ya miaka 10 ya NHIF tangu kuanzishwa kwake sherehe zilizofanyika Makao Makuu ya Mfuko huo.
“Tunaweza kutumia uzoefu kutoka nchi mbalimbali ambazo zimepiga hatua katika masuala ya Bima ya Afya lakini kwa kuzingatia utamaduni na mazingira ya kitanzania, kampeni za uhamasishaji ziwe endelevu kwa viongozi wa Serikali, wawakilishi wa wananchi na viongozi wa dini…wote tushiriki katika kampeni hii tukizingatia kuwa suala hili linamhusu kila mtu,” alisema Pinda.
Akizungumzia matumizi ya fedha za uchangiaji na uboreshaji wa Huduma, Fedha ambazo hulipwa na NHIF, alisema huelekezwa zaidi katika uboreshaji wa huduma nchini na mpaka sasa Mfuko huo umelipa zaidi ya sh. Bilioni 140 kwa vituo mbalimbali vilivyosajiliwa na Serikali, Mashirika ya Dini na binafsi.
Hata hivyo alisema kuwa pamoja na fedha hizo kulipwa kwa lengo hilo, huduma bado si za kuridhisha hatua iliyomfanya kumwagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kukagua matumizi ya malipo yatokanayo na uchangiaji wa huduma za afya zikiwemo za NHIF, tele kwa tele na papo kwa papo lengo ni kuhakikisha matumizi bora ya fedha za Mfuko na kutoa huduma bora zaidi.
“Wito wangu hasa kwa watoa huduma, mjipange vizuri zaidi ili kuboresha huduma zenu, muwe waadilifu ili mpate malipo halali…msijihusishe na madai ya kughushi yatakayotishia uhai wa Mfuko wetu na msiruhusu kuharibu mahusiano yaliyo kati yenu na Mfuko, eleweni kwamba maendeleo ya Mfuko ndio mkombozi kwa wananchi wetu,” alisema Pinda.
Pamoja na hayo, aliuopongeza uongozi wa Mfuko kwa kitendo cha kuwatambua waasisi wa Mfuko huo ambao wamesadia kuleta ufanisi na ustawi wa Mfuko hivyo akautaka kuendelea na utaratibu huo kwa kuwa unatoa hamasa kwa wengine kutoa mchango wao wa hali na mali katika kufanikisha malengo yaliyopo.
Naye Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa katika salaam zake aliutaka Mfuko kulinda mafanikio yaliyofikiwa, kufanya kazi kwa bidii na maarifa huku wakijua kuwa bado kuna kundi kubwa la Watanzania wanaohitaji huduma hasa vijijini.
‘Msiogope kuthubutu kufanya mambo yanayolenga kuboresha huduma za matibabu kwa watanzania hasa katika ujenzi wa vituo vya matibabu, kusaidia vifaa tiba na elimu zaidi ili uhai wa Mfuko ubaki kuwa imara,” alisema Rais Mkapa.
Aidha aliwataka wananchi kutodanganywa kuhusu afya zao hivyo suala la uchangiaji ni la muhimu na Bima ya Afya ndio mtindo wa sasa wa maisha.
Tuesday, February 21, 2012
RC: Ufanyeni Mradi wa KfW kuwa na tija
MKUU wa Mkoa Tanga Chiku Galawa amewataka viongozi mkoani humo kuhakikisha wanafanya uhamasishaji juu ya mradi wa Mama Mjamzito na Mtoto Mchanga unaofadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kupitia Benki ya Ujerumani (KfW) kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bimaya Afya ili mradi huo uweze kuwa tija.
Amesema ni lazima viongozi waamke na kuongeza mapambano ya kunusuru afya za akina mama wajawazito na watoto.
Galawa aliyasema hayo jana wakati wa uzinduzi wa Mradi huo ambao ulifanyika mkoani humo na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wafadhili wa Mradi huo, wakuu wa Wilaya, Uongozi kutoka Mkoa wa Mbeya, wanufaika wa mradi huo ambao ni akina mama wajawazito na wadau wengine.
“Uendelevu wa Mradi huu utatokana na juhudi za uelimishaji wa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii na Mfuko wa Taifa wa Bila ya Afya…natoa mwito kwa viongozi wenzangu wa Mkoa wa Tanga na Mbeya tuone fahari juu ya mradi huu muhimu na tujione wenye bahati miongoni mwa Watanzania,” alisema Galawa.
Alisema kuwa pamoja na juhudi mbalimbali ambazo zinafanywa na Serikali katika kukabiliana na changamoto za Sekta ya Afya lakini bado zimeendelea kuibuka zingine kutokana pia na kuongezeka kwa idadi watu hivyo Serikali peke yake ina mzigo mkubwa unaotakiwa kuungwa mkono na wadau wengine wa maendeleo.
“Kutokana na hali hiyo inayoikabili Serikali, daima tunaendelea kujivunia kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa kuwahudumia wananchi katika maeneo tofauti ya nchi yetu kulingana na makundi yao,” alisema na kuongeza.
“Ni kazi hiyo nzuri inayofanywa na Mfuko huu ambayo imewezesha Wafadhili kutoka Serikali ya Ujerumani (KfW) kukubali kuunga mkono juhudi hizo na sasa kwa ajili ya wanawake wajawazito na watoto wachanga katika mikoa ya Tanga na Mbeya,” alisema Galawa.
Alisema mradi huo unaolenga kuboresha huduma za afya hasa kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga utasaidia akina mama kujifungua katika mazingira ya uangalizi zaidi na kuepukana na madhara ambayo wangeweza kuyapata kutokana na kujifungulia majumbani.
Galawa pia alieleza kuwa moja ya faida za mradi huo ni pamoja na kutoa vifaa tiba kama vile vitanda vya kujifungulia na vingine hivyo hatua hiyo itasaidia kutokana na ukweli kwamba vituo vingi vinakabiliwa na upungufu wa vifaa tiba.
“Ni matumaini yangu kuwa watoa huduma wa mikoa hii mtazingatia matumizi bora ya vifaa hivyo ili view endelevu na hasa kwa malengo yaliyokusudiwa,” alisema Galawa.
Kutokana na hali hiyo, aliwataka viongozi wa Halmashauri wakiongozwa na Madiwani watatekeleza wajibu wao wa kuhakikisha kwamba mradi huo unakuwa na tija na utambuzi wa akina mama hao unafanywa kwa uwazi bila upendeleo ili lengo la kuhakikisha uzazi salama kwa wanawake linatimia.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Emanuel Humba alisema kuwa lengo kubwa la mradi huo ni kuwawezesha akina mama wasio na uwezo kupata huduma za matibabu kupitia utaratibu wa NHIF katika kipindi chote cha ujauzito na miezi mitatu baada ya kujifungua.
Aidha mradi huo utasaidia kuzilipia kaya za akina mama hao mchango wa Mfuko wa Afya ya Jamii kwa kipindi cha mwaka mmoja, kuwajengea uwezo wa kifedha watoa huduma zitokanazo na Bima ya Afya.
Humba alisema kuwa mradi huo ulianza kutekelezwa katika Wilaya ya Korogwe, Pangani, Ileje na Rungwe kwa kuwaandikisha wajawazito na kuwapatia vitambulisho vya Bima ya Afya, usambazaji wa fomu 12,700 za kuandikisha walengwa ambapo mpaka hivi sasa jumla ya akina mama 600 wameshajitokeza na kuanza kufaidika.
Kutokana na hayo, Humba aliwaomba viiongozi wote wakiwemo wabunge kuhakikisha wanasaidia suala la uhamasishaji ili akina mama wengi zaidi na wasio na uwezo waweze kunufaika na Mradi huo.
Naye Mwakilishi wa KfW, Dk Kai Gesing alisema kuwa suala la afya ni suala nyeti sana hasa katika kuwasaidia akina mama wajawazito na watoto hivyo kwa kulitambua hilo, wakaona umuhimu wa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya katika kutekeleza Mradi huo.
"Suala la akina mama ni suala nyeti sana na ndio maana tumeamua kuja na Mradi huu ili hatimaye tupunguze idadi ya vifo vya akina mama hawa lakini pia kuhakikisha wengi wanajifungulia katika vituo vya afya na kwenye mazingira mazuri," alisema Dk Gesing.
Kwa upande wa wanufaika wa mradi huo ambao ni akina mama wajawazito, waliupongeza Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya pamoja na wafadhili wa mradi huo kwa kuleta mradi huo ambao wao wanauona ni mkombozi wa afya zao pamoja na familia zao ambazo zitanufaika kwa matibabu kupitia CHF.
Amesema ni lazima viongozi waamke na kuongeza mapambano ya kunusuru afya za akina mama wajawazito na watoto.
Galawa aliyasema hayo jana wakati wa uzinduzi wa Mradi huo ambao ulifanyika mkoani humo na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wafadhili wa Mradi huo, wakuu wa Wilaya, Uongozi kutoka Mkoa wa Mbeya, wanufaika wa mradi huo ambao ni akina mama wajawazito na wadau wengine.
“Uendelevu wa Mradi huu utatokana na juhudi za uelimishaji wa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii na Mfuko wa Taifa wa Bila ya Afya…natoa mwito kwa viongozi wenzangu wa Mkoa wa Tanga na Mbeya tuone fahari juu ya mradi huu muhimu na tujione wenye bahati miongoni mwa Watanzania,” alisema Galawa.
Alisema kuwa pamoja na juhudi mbalimbali ambazo zinafanywa na Serikali katika kukabiliana na changamoto za Sekta ya Afya lakini bado zimeendelea kuibuka zingine kutokana pia na kuongezeka kwa idadi watu hivyo Serikali peke yake ina mzigo mkubwa unaotakiwa kuungwa mkono na wadau wengine wa maendeleo.
“Kutokana na hali hiyo inayoikabili Serikali, daima tunaendelea kujivunia kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa kuwahudumia wananchi katika maeneo tofauti ya nchi yetu kulingana na makundi yao,” alisema na kuongeza.
“Ni kazi hiyo nzuri inayofanywa na Mfuko huu ambayo imewezesha Wafadhili kutoka Serikali ya Ujerumani (KfW) kukubali kuunga mkono juhudi hizo na sasa kwa ajili ya wanawake wajawazito na watoto wachanga katika mikoa ya Tanga na Mbeya,” alisema Galawa.
Alisema mradi huo unaolenga kuboresha huduma za afya hasa kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga utasaidia akina mama kujifungua katika mazingira ya uangalizi zaidi na kuepukana na madhara ambayo wangeweza kuyapata kutokana na kujifungulia majumbani.
Galawa pia alieleza kuwa moja ya faida za mradi huo ni pamoja na kutoa vifaa tiba kama vile vitanda vya kujifungulia na vingine hivyo hatua hiyo itasaidia kutokana na ukweli kwamba vituo vingi vinakabiliwa na upungufu wa vifaa tiba.
“Ni matumaini yangu kuwa watoa huduma wa mikoa hii mtazingatia matumizi bora ya vifaa hivyo ili view endelevu na hasa kwa malengo yaliyokusudiwa,” alisema Galawa.
Kutokana na hali hiyo, aliwataka viongozi wa Halmashauri wakiongozwa na Madiwani watatekeleza wajibu wao wa kuhakikisha kwamba mradi huo unakuwa na tija na utambuzi wa akina mama hao unafanywa kwa uwazi bila upendeleo ili lengo la kuhakikisha uzazi salama kwa wanawake linatimia.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Emanuel Humba alisema kuwa lengo kubwa la mradi huo ni kuwawezesha akina mama wasio na uwezo kupata huduma za matibabu kupitia utaratibu wa NHIF katika kipindi chote cha ujauzito na miezi mitatu baada ya kujifungua.
Aidha mradi huo utasaidia kuzilipia kaya za akina mama hao mchango wa Mfuko wa Afya ya Jamii kwa kipindi cha mwaka mmoja, kuwajengea uwezo wa kifedha watoa huduma zitokanazo na Bima ya Afya.
Humba alisema kuwa mradi huo ulianza kutekelezwa katika Wilaya ya Korogwe, Pangani, Ileje na Rungwe kwa kuwaandikisha wajawazito na kuwapatia vitambulisho vya Bima ya Afya, usambazaji wa fomu 12,700 za kuandikisha walengwa ambapo mpaka hivi sasa jumla ya akina mama 600 wameshajitokeza na kuanza kufaidika.
Kutokana na hayo, Humba aliwaomba viiongozi wote wakiwemo wabunge kuhakikisha wanasaidia suala la uhamasishaji ili akina mama wengi zaidi na wasio na uwezo waweze kunufaika na Mradi huo.
Naye Mwakilishi wa KfW, Dk Kai Gesing alisema kuwa suala la afya ni suala nyeti sana hasa katika kuwasaidia akina mama wajawazito na watoto hivyo kwa kulitambua hilo, wakaona umuhimu wa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya katika kutekeleza Mradi huo.
"Suala la akina mama ni suala nyeti sana na ndio maana tumeamua kuja na Mradi huu ili hatimaye tupunguze idadi ya vifo vya akina mama hawa lakini pia kuhakikisha wengi wanajifungulia katika vituo vya afya na kwenye mazingira mazuri," alisema Dk Gesing.
Kwa upande wa wanufaika wa mradi huo ambao ni akina mama wajawazito, waliupongeza Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya pamoja na wafadhili wa mradi huo kwa kuleta mradi huo ambao wao wanauona ni mkombozi wa afya zao pamoja na familia zao ambazo zitanufaika kwa matibabu kupitia CHF.
NHIF yazindua Mradi wa akina mama wajawazito na watoto wachanga Tanga
![]() |
| Akikabidhi kadi kwa akina mama wanaonufaika na mradi huo. |
![]() |
| Mkuu wa Mkoa akiangalia vitambulisho vilivyotolewa na NHIF akiwa na viongozi wa Mkoa wa Tanga na Mbeya ambako Mradi huu unatekelezwa pamoja na wafadhili wa mradi huo. |
![]() |
| Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Bi. Zipora akipokea vitambulisho vya akina mama wajawazito wilayani kwake. |
Subscribe to:
Posts (Atom)





