* Asema Tanzania itafanya mambo bila shinikizo
* Asema wakoloni waliiacha nchi ikiwa hoi
* Atamba hatua zilizofikiwa, asisitiza kuchapa kazi
* Atamba 2015 Tanzania itakuwa na Jeshi la Mfano
Na Grace Michael
RAIS Jakaya Kikwete jana aliwaongoza Watanzania katika maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru huku akisisitiza kuwa kamwe Tanzania haitaamliwa mambo yake na nchi nyingine.
Alisema kuwa amani, utulivu, mshikamano wa Watanzania ni mafanikio makubwa yaliyotokana na sera nzuri zilizoanzishwa na waasisi wa nchi hii akiwemo Mwalimu Julius Nyerere pamoja na viongozi waliofutia akiwemo Ally Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na yeye mwenyewe.
Kauli hiyo aliitoa katika maadhimisho hayo Dar es Salaam katika uwanja wa Uhuru ambapo, Rais Kikwete aliamua kuzungumza kutokana na umuhimu wa siku ya jana ambayo ilikuwa ni kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania Bara.
"Niwahakikishie tu Watanzania wenzangu kuwa katika mambo tutakayoyafanya kamwe hatutaamuliwa na mtu yoyote...tutafanya tunachokiamua wenyewe kwani tunayo amani, utulivu, mshikamano na ni nchi ya aina yake," alisema Rais Kikwete.
Alisema kuwa katika safari ya miaka 50 ya uhuru nchi imepita katika changamoto mbalimbali na katika maadui watatu waliotangazwa baada ya kupata uhuru ambao ni umasikini, ujinga na maradhi nchi imepiga hatua katika mapambano dhidi ya maadui hao.
"Tuna mafanikio makubwa tena ya kujivunia ikilinganishwa na tulivyoachwa na wakoloni...walituacha weupe kabisa na kama barabara za lami waliacha ziko tatu tu ambazo ni Moshi- Arusha, Tanga- Korogwe na Dar es Salaam- Morogoro...walitugawa walipo wao ndio kulikuwa na umeme, maji na lami lakini mtanzania alipo kama ni maji alipata ya debe," alisema Rais Kikwete.
Alisema kuwa pamoja na wakoloni kuiacha nchi ikiwa hoi lakini uongozi uliokuwepo baada ya uhuru na mpaka sasa umeweza kufanya kazi kubwa hali inayomwezesha Mtanzania kufika mahali popote kwa muda mfupi tofauti na hapo awali.
Alisema pamoja na mafanikio hayo, kama nchi bado kuna kazi ya kufanya kutokana na kasi ya mabadiliko na changamoto zilizopo hivi sasa hivyo kama Watanzania akawataka kuongeza bidii katika utendaji kazi ili kuweza kwenda sambamba na matarajio ya nchi.
"Niwakumbushe tu ambao hawalijui hili...waingereza hawakuacha chochote hivyo wananchi kamwe msivunjike moyo bado tuna kazi ya kufanya na cha kujivunia katika kipindi hiki tuna msingi mzuri," alisema Rais Kikwete.
Katika hatua nyingine Rais Kikwete aliwapongeza viongozi walioandaa na kuratibu maadhimisho hayo akiwemo Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Akizungumzia shamra shamra zilizokuwepo katika maadhimisho hayo, alilipongeza gwaride kwa namna lilivyojipanga lakini pia kuoneshwa kwa zana mbalimbali za kivita ambazo zinaonesha wazi kuwa nchi iko na zana za kutosha katika kuhakikisha ulinzi wake uko salama.
"Nadhani kila mmoja amejionea hapa vifaa na zana mbalimbali za kivita na hivyo ni baadhi tu kwani vingekuja vyote hapa pasingetosha na tunazidi kujiimarisha na ifikapo 2015 nchi yetu itakuwa na Jeshi la ambalo halikuwa na mfano," alisema Rais Kikwete.
Alisema kuwa kama Tanzania inayo mambo mengi ya kujivunia ambayo yameweka historia likiwemo la kupigana na kulisambaratisha Jeshi la Uganda hivyo hiyo ni ishara tosha kuwa Tanzania iko imara na itaendelea kuwa hivyo ili kuweza kulinda misingi iliyoachwa ikiwemo ya amani na utulivu.
Hata hivyo Rais Kikwete alitumia mwanya huo kuwakumbuka waasisi 17 ambao walikuwa mbele katika kupigania uhuru wa Tanzania Bara ambao alisisitiza kuwa kama nchi tunao wajibu wa kuwapa heshima kutokana na walichokifanya katika kipindi hicho.
"Ni lazima kuwatambua na kuwakumbuka kwa uamuzi wao wa kishujaa wa kudai uhuru wa nchi hii na kati ya waasisi hao 17 ni watatu tu ndio wapo hai na wengine 14 wametangulia mbele za haki...ni wajibu wetu kutoa heshima kwao kwani walifanya kazi kubwa," alisema.
Kutokana na hali hiyo, Rais Kikwete aliwaambia Watanzania kuwa katika miaka 50 ya uhuru ni dhahiri kuwa "Tumethubutu, Tumeweza na tunaendelea kusonga mbele".
Maadhimisho hayo mbali na wananchi kutoka katika maeneo mbalimbali ya Tanzania, yalihudhuriwa na viongozi wa kitaifa wa ndani na nje wakiwemo marais wa nchi zingine ambapo Rais Kikwete alisema hiyo ni ishara ya ushirikiano ambapo aliahidi kuuendeleza.
Friday, December 9, 2011
NHIF yaweka historia miaka 50 ya Uhuru
Na Grace Michael
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya umeandika historia ndani ya miaka 50 ya uhuru kwa kuibuka mshindi wa kwanza wa ujumla Barani Afrika kwa Taasisi na Mashirika yanayotoa huduma za Hifadhi ya Jamii.
Ushindi huo umeufanya Mfuko huo kutunukiwa vyeti vitatu vya heshima kwa umahiri na jitihada za kuboresha huduma bora katika maeneo mbalimbali.
Akizungumzia ushindi huo Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Emmanuel Humba, alisema kuwa ushindi huo si wa mfuko pekee bali umeleta heshima ya nchi nzima na Watanzania wake kwa ujumla.
Humba aliyataja maeneo ambayo yameufanya mfuko huo kuibuka kidedea ni pamoja na usimamizi wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) hasa kwenye kasi ya kuongezeka kwa wanaohudumiwa na mfuko huo katika kipindi kifupi tangu Serikali ilipokasimu madaraka kwa NHIF.
Huduma ya Vifaa tiba na watoa huduma na utoaji wa huduma uliowezesha kuboresha huduma na kupunguza ukubwa wa tatizo la dawa na vifaa tiba hivyo kutoa mchango muhimu katika maendeleo ya sekta ya afya nchini nalo ni eneo jingine ambalo liliufanya mfuko huo kutunukiwa vyeti.
"Utoaji wa mafao na kusogeza huduma za Mfuko karibu na wanachama wake kupitia ufunguzi wa ofisi za kanda nao uliwafanya wenzetu wa Taasisi ya Kimataifa ya Mashirika ya Hifadhi ya Jamii Duniani, (ISSA) kuona tunafaa kupata vyeti hivyo," alisema Humba.
Alisema tuzo hiyo ilitolewa mjini Arusha mapema wiki hii na Rais wa ISSA, Errol Frank kwenye mkutano wa wakuu wa mashirika ya pesheni na Bima za Afya kanda ya Afrika na NHIF iliwakilishwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji Eugen Mikongoti.
Hata hivyo NHIF iliwahi kupata tuzo ya heshima kutoka kwa ISSA mwaka 2008, hivyo Humba akasema tuzo hiyo ina maana kubwa kwa mfuko kwa kuwa umeweza kuonesha kuwa umethubutu na umeweza.
"Tuzo hii imekuja wakati mwafaka kwani umedhihirisha kuwa ndani ya miaka 50 ya uhuru tumeweza...hii ni heshima kubwa kwa nchi na Mamlaka inayosimamia Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), lakini pia kwa wizara yetu ya Afya," alisema Humba.
Alisema kuwa mfuko unaamini kuwa imepata tuzo hiyo kutokana na mazingira na utamaduni wa Watanzania kujadiliana changamoto na kuzipatia ufumbuzi kwa pamoja na hivyo imefanikisha nchi kuonekana ni kivutio kwa mataifa mengine barani Afrika.
"Matarajio ya mfuko ni kuendelea kuzifanyia kazi changamoto za uboreshaji wa huduma...huduma za NHIF na CHF tunataka zifike ngazi ya chini kabisa ili wanachama waone umuhimu au faida za kujiunga...mtaji wa mtu yeyote ni afya yake hivyo kama mfuko hatuchezi na afya ya Mtanzania," alisema Humba.
Kutokana na hali hiyo, Humba alisema kuwa atakabidhi tuzo hiyo serikalini kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo ndiyo mama na mafanikio hayo yamepatikana kutokana na uongozi na ulezi mzuri.
"Nawashukuru sana Watanzania na wanachama wote kwa ujumla, tutaendelea kutambua mchango wenu kwa kuwapa huduma iliyo bora zaidi...tuna mafao ambayo nchi zingine zimeshindwa kuyatoa kwa wanachama wake," alisema Humba.
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya umeandika historia ndani ya miaka 50 ya uhuru kwa kuibuka mshindi wa kwanza wa ujumla Barani Afrika kwa Taasisi na Mashirika yanayotoa huduma za Hifadhi ya Jamii.
Ushindi huo umeufanya Mfuko huo kutunukiwa vyeti vitatu vya heshima kwa umahiri na jitihada za kuboresha huduma bora katika maeneo mbalimbali.
Akizungumzia ushindi huo Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Emmanuel Humba, alisema kuwa ushindi huo si wa mfuko pekee bali umeleta heshima ya nchi nzima na Watanzania wake kwa ujumla.
Humba aliyataja maeneo ambayo yameufanya mfuko huo kuibuka kidedea ni pamoja na usimamizi wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) hasa kwenye kasi ya kuongezeka kwa wanaohudumiwa na mfuko huo katika kipindi kifupi tangu Serikali ilipokasimu madaraka kwa NHIF.
Huduma ya Vifaa tiba na watoa huduma na utoaji wa huduma uliowezesha kuboresha huduma na kupunguza ukubwa wa tatizo la dawa na vifaa tiba hivyo kutoa mchango muhimu katika maendeleo ya sekta ya afya nchini nalo ni eneo jingine ambalo liliufanya mfuko huo kutunukiwa vyeti.
"Utoaji wa mafao na kusogeza huduma za Mfuko karibu na wanachama wake kupitia ufunguzi wa ofisi za kanda nao uliwafanya wenzetu wa Taasisi ya Kimataifa ya Mashirika ya Hifadhi ya Jamii Duniani, (ISSA) kuona tunafaa kupata vyeti hivyo," alisema Humba.
Alisema tuzo hiyo ilitolewa mjini Arusha mapema wiki hii na Rais wa ISSA, Errol Frank kwenye mkutano wa wakuu wa mashirika ya pesheni na Bima za Afya kanda ya Afrika na NHIF iliwakilishwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji Eugen Mikongoti.
Hata hivyo NHIF iliwahi kupata tuzo ya heshima kutoka kwa ISSA mwaka 2008, hivyo Humba akasema tuzo hiyo ina maana kubwa kwa mfuko kwa kuwa umeweza kuonesha kuwa umethubutu na umeweza.
"Tuzo hii imekuja wakati mwafaka kwani umedhihirisha kuwa ndani ya miaka 50 ya uhuru tumeweza...hii ni heshima kubwa kwa nchi na Mamlaka inayosimamia Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), lakini pia kwa wizara yetu ya Afya," alisema Humba.
Alisema kuwa mfuko unaamini kuwa imepata tuzo hiyo kutokana na mazingira na utamaduni wa Watanzania kujadiliana changamoto na kuzipatia ufumbuzi kwa pamoja na hivyo imefanikisha nchi kuonekana ni kivutio kwa mataifa mengine barani Afrika.
"Matarajio ya mfuko ni kuendelea kuzifanyia kazi changamoto za uboreshaji wa huduma...huduma za NHIF na CHF tunataka zifike ngazi ya chini kabisa ili wanachama waone umuhimu au faida za kujiunga...mtaji wa mtu yeyote ni afya yake hivyo kama mfuko hatuchezi na afya ya Mtanzania," alisema Humba.
Kutokana na hali hiyo, Humba alisema kuwa atakabidhi tuzo hiyo serikalini kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo ndiyo mama na mafanikio hayo yamepatikana kutokana na uongozi na ulezi mzuri.
"Nawashukuru sana Watanzania na wanachama wote kwa ujumla, tutaendelea kutambua mchango wenu kwa kuwapa huduma iliyo bora zaidi...tuna mafao ambayo nchi zingine zimeshindwa kuyatoa kwa wanachama wake," alisema Humba.
Miaka 50 ya uhuru tutafakari zaidi
Na Grace Michael
NAJISIKIA furaha kuona nchi yangu ikiadhimisha miaka 50 ya uhuru wake.
Nafarijika kwa kuwa nchi yangu ni kisima cha amani, imejaa utulivu tofauti na nchi zingine.
Nafurahi kuwaona Watanzania leo hii wakiandika historia kubwa ya muda wa miaka hiyo 50 tangu wapate uhuru wao, ambapo mbali na mambo mengine nchi imefanikiwa kupiga hatua katika nyanja mbalimbali.
Wakati tunaadhimisha maadhimisho haya ni vyema Watanzania tukatumia fursa hii kutafakari tulikotoka, tulipo na tunakokwenda.
Nasema hivyo kwa kuwa bila tafakari hiyo kamwe hatuwezi kufanya lolote katika safari inayoanza kesho ya miaka mingine 50 ya uhuru wetu.
Ikumbukwe kuwa pamoja na utulivu na amani iliyopo hapa nchini, lakini nchi ipo katika kipindi kigumu kwa kuwa yapo matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi ambayo kama hayatapatiwa ufumbuzi wa haraka tunaweza kubaki na utulivu tu lakini amani ikatoweka.
Ili mwananchi awe na amani ni lazima awe na uhakika wa maisha yake kwa mfano, vijana kuwa na uhakika wa ajira, wananchi kutokuwa na umasikini, upatikanaji wa huduma zote za kijamii uwepo wakati wote pamoja na familia za Watanzania kuwa na uhakika wa kuendesha maisha yake ya kila siku.
Kwa hali ya kawaida huwezi ukasema una amani huku huna fedha ya kugharamia matibabu ya mwanao au mwana familia wako, huwezi kuwa na amani wakati familia yako ikishinda na njaa, watoto kukosa huduma za elimu na mambo mengine mengi.
Hivyo pamoja na sifa kubwa iliyopo hapa nchini ambayo ni ya kudumisha amani, lakini ni vyema sasa wakati tukiadhimisha maadhimisho haya, Serikali ikafanya kila linalowezekana kuhakikisha inaweka mazingira rafiki kwa wananchi wake ili wapate vitu vya msingi ambavyo vitawafanya wadumishe hiyo amani.
Lakini pamoja na Serikali kuwa na mzigo wa kuweka mazingira hayo rafiki, na sisi kama wananchi tunao mzigo wa kuhakikisha tunafanya kazi zenye tija na si kukaa vibarazani tukitarajia Serikali ilete kila kitu.
Natambua nchi sasa iko katika mfumko mkubwa wa bei, wananchi wake wana umasikini mkubwa, tha
mani ya shilingi yetu imeshuka thamani mambo yote hayo yanasababisha kuongezeka kwa ugumu wa maisha.
Kutokana na hayo yote, kamwe tusije kudanganyika tukaipoteza amani na utulivu ambao viongozi waliopita walivilinda kwa gharama kubwa.
Nalazimika kusema hivyo kwani huwezi ukafanya kazi zozote za uzalishaji au maendeleo ukiwa katika migogoro au vita hivyo kwa maana hiyo ni lazima tuhakikishe amani iliyopo inalindwa.
Natambua hivi sasa Watanzania wanao uelewa mkubwa katika mambo mbalimbali ambao natarajia kila mmoja kwa nafasi yake atautumia katika kuijenga nchi yetu na si kuibomoa.
Mungu Tubariki Watanzania.
0782 35 66 88
NAJISIKIA furaha kuona nchi yangu ikiadhimisha miaka 50 ya uhuru wake.
Nafarijika kwa kuwa nchi yangu ni kisima cha amani, imejaa utulivu tofauti na nchi zingine.
Nafurahi kuwaona Watanzania leo hii wakiandika historia kubwa ya muda wa miaka hiyo 50 tangu wapate uhuru wao, ambapo mbali na mambo mengine nchi imefanikiwa kupiga hatua katika nyanja mbalimbali.
Wakati tunaadhimisha maadhimisho haya ni vyema Watanzania tukatumia fursa hii kutafakari tulikotoka, tulipo na tunakokwenda.
Nasema hivyo kwa kuwa bila tafakari hiyo kamwe hatuwezi kufanya lolote katika safari inayoanza kesho ya miaka mingine 50 ya uhuru wetu.
Ikumbukwe kuwa pamoja na utulivu na amani iliyopo hapa nchini, lakini nchi ipo katika kipindi kigumu kwa kuwa yapo matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi ambayo kama hayatapatiwa ufumbuzi wa haraka tunaweza kubaki na utulivu tu lakini amani ikatoweka.
Ili mwananchi awe na amani ni lazima awe na uhakika wa maisha yake kwa mfano, vijana kuwa na uhakika wa ajira, wananchi kutokuwa na umasikini, upatikanaji wa huduma zote za kijamii uwepo wakati wote pamoja na familia za Watanzania kuwa na uhakika wa kuendesha maisha yake ya kila siku.
Kwa hali ya kawaida huwezi ukasema una amani huku huna fedha ya kugharamia matibabu ya mwanao au mwana familia wako, huwezi kuwa na amani wakati familia yako ikishinda na njaa, watoto kukosa huduma za elimu na mambo mengine mengi.
Hivyo pamoja na sifa kubwa iliyopo hapa nchini ambayo ni ya kudumisha amani, lakini ni vyema sasa wakati tukiadhimisha maadhimisho haya, Serikali ikafanya kila linalowezekana kuhakikisha inaweka mazingira rafiki kwa wananchi wake ili wapate vitu vya msingi ambavyo vitawafanya wadumishe hiyo amani.
Lakini pamoja na Serikali kuwa na mzigo wa kuweka mazingira hayo rafiki, na sisi kama wananchi tunao mzigo wa kuhakikisha tunafanya kazi zenye tija na si kukaa vibarazani tukitarajia Serikali ilete kila kitu.
Natambua nchi sasa iko katika mfumko mkubwa wa bei, wananchi wake wana umasikini mkubwa, tha
mani ya shilingi yetu imeshuka thamani mambo yote hayo yanasababisha kuongezeka kwa ugumu wa maisha.
Kutokana na hayo yote, kamwe tusije kudanganyika tukaipoteza amani na utulivu ambao viongozi waliopita walivilinda kwa gharama kubwa.
Nalazimika kusema hivyo kwani huwezi ukafanya kazi zozote za uzalishaji au maendeleo ukiwa katika migogoro au vita hivyo kwa maana hiyo ni lazima tuhakikishe amani iliyopo inalindwa.
Natambua hivi sasa Watanzania wanao uelewa mkubwa katika mambo mbalimbali ambao natarajia kila mmoja kwa nafasi yake atautumia katika kuijenga nchi yetu na si kuibomoa.
Mungu Tubariki Watanzania.
0782 35 66 88
Sumaye: Rushwa, ufisadi ni janga
* Ataka vita dhidi yake ipiganwe kwa pamoja
* Aifunda Chadema kuhusu Katiba Mpya
Na Grace Michael
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye amesema kuwa bila kuwa na vita ya dhati na ya pamoja dhidi ya mapambano rushwa na ufisadi nchi itaangamia.
Sumaye aliyasema hayo Dar es Salaam jana katika maonesho ya maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru ynayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere.
"Rushwa na ufisadi ni mambo yanayoangamiza Taifa letu na kama hatukuwa na umoja katika kupambana navyo Taifa litakwisha...vita hii isiachwe kwa Raifa peke yake tuipigane wote," alisema.
Alisema kuwa rushwa ni kikwazo kikubwa katika kuyafikia maendeleo ya kweli kwa kuwa ndiyo inasababisha kupokwa kwa haki za wanyonge, kutekelezwa kwa miradi chini ya kiwango, kupewa kazi mtu asiye na sifa za kufanya kazi hiyo hatua inayosababisha wananchi kuichukia hata Serikali yao.
Kutokana na hali hiyo aliwaomba Watanzania kuhakikisha mambo mabaya wanayapinga kwa uwazi ili yaweze kuachwa kwa maslahi ya umma.
*Asisitiza kulinda amani
Katika hatua nyingine, Sumaye alisema kuwa pamoja na matatizo ya umasikini ambayo bado yanawakabili wananchi wa Tanzania lakini kuna haja kubwa ya kuhakikisha amani inalindwa kwa nguvu zote.
"Nakubali kabisa kuwa unaweza ukakosa amani hata kama eneo lako halina vita, huwezi ukawa na amani huku ukiwa na matatizo ya njaa, huduma za msingi lakini ni lazima tutambue kuwa tunatakiwa kufanya kazi kufa na kupona ili kujikwamua na hali hii, hakuna Serikali inayoweza kumgawia mwananchi wake fedha bali inaweka mazingira mazuri," alisema.
Kutokana na hali hiyo alisisitiza kuwa ni lazima viangaliwe vitu vyote vinavyoweza kusababisha kutoweka kwa amani miongoni mwa wananchi ili vifanyiwe kazi na hatimaye amani iliyopo kubaki kama ilivyo.
Hata hivyo alisema kuwa Serikali inafanya juhudi mbalimbali katika kuhakikisha wananchi wake wanaachana na umasikini ikiwemo ya kutoa kipaumbele katika suala la kilimo ambalo linahusisha asilimia kubwa ya Watanzania.
*Anena kuhusu Katiba
Akizungumzia mchakato wa katiba ulivyo sasa, alisema kuwa hakuna haja ya kuwepo kwa malumbano katika hatua hizi za awali na ambazo zimefanyika kwa taratibu zinazotakiwa.
Alisema kuwa hoja zote zinazojadiliwa bungeni zinatakiwa kushindana kwa hoja na baada ya kutoka huko na kuwa mikononi mwa Rais ni vigumu kutengua hatua inayofuata.
"Kama kuna mbunge anapingana na hoja...ndo muda anaotakiwa kupambana na hoja hiyo bungeni huku wananchi wakimsikiliza lakini mbunge unapotoka kwa kususia hoja hiyo si njia sahihi sana kwani muswada huo ulipishwa bungeni na hatua iliyofuata ni Rais kutia saini na si vinginevyo," alisema.
Hata hivyo alisema kuwa hatua ambayo ni ya muhimu katika mchakato huo ni ya wananchi kutoa mawazo au maoni yao na si hatua hii hivyo akasema hakuna haja ya kulumbana kwa kuwa hata Serikali si mlemavu wa kusikia vilio vya wananchi hasa katika suala hili la Katiba.
*Umoja wa Kitaifa
Katika suala hilo, Sumaye alisema kuwa ni wakati wa Watanzania kukiri kuwa Umoja bado uko imara pamoja na kuwepo kwa mabadiliko ya mambo mbalimbali.
*Kupambana na umasikini, ujinga na Maradhi
Sumaye alisema kuwa katika kupambana na maadui hao watatu ambao walitangazwa mara tu baada ya kupata uhuru yapo mafanikio ambayo yamefikiwa pamoja na kuwepo kwa changamoto mbalimbali.
Kuhusu umasikini alisema kuwa ni lazima Watanzania kwa sasa tufanye kazi bila huruma ili tuweze kupambana na adui huyo.
Hata hivyo alisema kuwa changamoto alizopambana nazo Mwalimu Julius Nyerere ni tofauti kabisa na changamoto anazopambana nazo Rais Jakaya Kikwete kwa kuwa mambo mengi yamebadilika.
"Huwa najiuliza sijui Mwalimu alipataje hata Baraza la Mawaziri kwa kuwa watu walikuwa wachache lakini leo kuna wasomi wengi na ndio maana nasema yapo mabadiliko makubwa ambayo yamekuja na changamoto zake ambazo tunatakiwa kwa pamoja kupambana nazo," alisema Sumaye.
Alitumia mwanya huo kumpongeza Rais Kikwete kwa kuandaa utaratibu mzuri wa maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru ambao umewezesha wananchi kupata historia ya nchi yao kabla na baada ya uhuru.
* Aifunda Chadema kuhusu Katiba Mpya
Na Grace Michael
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye amesema kuwa bila kuwa na vita ya dhati na ya pamoja dhidi ya mapambano rushwa na ufisadi nchi itaangamia.
Sumaye aliyasema hayo Dar es Salaam jana katika maonesho ya maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru ynayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere.
"Rushwa na ufisadi ni mambo yanayoangamiza Taifa letu na kama hatukuwa na umoja katika kupambana navyo Taifa litakwisha...vita hii isiachwe kwa Raifa peke yake tuipigane wote," alisema.
Alisema kuwa rushwa ni kikwazo kikubwa katika kuyafikia maendeleo ya kweli kwa kuwa ndiyo inasababisha kupokwa kwa haki za wanyonge, kutekelezwa kwa miradi chini ya kiwango, kupewa kazi mtu asiye na sifa za kufanya kazi hiyo hatua inayosababisha wananchi kuichukia hata Serikali yao.
Kutokana na hali hiyo aliwaomba Watanzania kuhakikisha mambo mabaya wanayapinga kwa uwazi ili yaweze kuachwa kwa maslahi ya umma.
*Asisitiza kulinda amani
Katika hatua nyingine, Sumaye alisema kuwa pamoja na matatizo ya umasikini ambayo bado yanawakabili wananchi wa Tanzania lakini kuna haja kubwa ya kuhakikisha amani inalindwa kwa nguvu zote.
"Nakubali kabisa kuwa unaweza ukakosa amani hata kama eneo lako halina vita, huwezi ukawa na amani huku ukiwa na matatizo ya njaa, huduma za msingi lakini ni lazima tutambue kuwa tunatakiwa kufanya kazi kufa na kupona ili kujikwamua na hali hii, hakuna Serikali inayoweza kumgawia mwananchi wake fedha bali inaweka mazingira mazuri," alisema.
Kutokana na hali hiyo alisisitiza kuwa ni lazima viangaliwe vitu vyote vinavyoweza kusababisha kutoweka kwa amani miongoni mwa wananchi ili vifanyiwe kazi na hatimaye amani iliyopo kubaki kama ilivyo.
Hata hivyo alisema kuwa Serikali inafanya juhudi mbalimbali katika kuhakikisha wananchi wake wanaachana na umasikini ikiwemo ya kutoa kipaumbele katika suala la kilimo ambalo linahusisha asilimia kubwa ya Watanzania.
*Anena kuhusu Katiba
Akizungumzia mchakato wa katiba ulivyo sasa, alisema kuwa hakuna haja ya kuwepo kwa malumbano katika hatua hizi za awali na ambazo zimefanyika kwa taratibu zinazotakiwa.
Alisema kuwa hoja zote zinazojadiliwa bungeni zinatakiwa kushindana kwa hoja na baada ya kutoka huko na kuwa mikononi mwa Rais ni vigumu kutengua hatua inayofuata.
"Kama kuna mbunge anapingana na hoja...ndo muda anaotakiwa kupambana na hoja hiyo bungeni huku wananchi wakimsikiliza lakini mbunge unapotoka kwa kususia hoja hiyo si njia sahihi sana kwani muswada huo ulipishwa bungeni na hatua iliyofuata ni Rais kutia saini na si vinginevyo," alisema.
Hata hivyo alisema kuwa hatua ambayo ni ya muhimu katika mchakato huo ni ya wananchi kutoa mawazo au maoni yao na si hatua hii hivyo akasema hakuna haja ya kulumbana kwa kuwa hata Serikali si mlemavu wa kusikia vilio vya wananchi hasa katika suala hili la Katiba.
*Umoja wa Kitaifa
Katika suala hilo, Sumaye alisema kuwa ni wakati wa Watanzania kukiri kuwa Umoja bado uko imara pamoja na kuwepo kwa mabadiliko ya mambo mbalimbali.
*Kupambana na umasikini, ujinga na Maradhi
Sumaye alisema kuwa katika kupambana na maadui hao watatu ambao walitangazwa mara tu baada ya kupata uhuru yapo mafanikio ambayo yamefikiwa pamoja na kuwepo kwa changamoto mbalimbali.
Kuhusu umasikini alisema kuwa ni lazima Watanzania kwa sasa tufanye kazi bila huruma ili tuweze kupambana na adui huyo.
Hata hivyo alisema kuwa changamoto alizopambana nazo Mwalimu Julius Nyerere ni tofauti kabisa na changamoto anazopambana nazo Rais Jakaya Kikwete kwa kuwa mambo mengi yamebadilika.
"Huwa najiuliza sijui Mwalimu alipataje hata Baraza la Mawaziri kwa kuwa watu walikuwa wachache lakini leo kuna wasomi wengi na ndio maana nasema yapo mabadiliko makubwa ambayo yamekuja na changamoto zake ambazo tunatakiwa kwa pamoja kupambana nazo," alisema Sumaye.
Alitumia mwanya huo kumpongeza Rais Kikwete kwa kuandaa utaratibu mzuri wa maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru ambao umewezesha wananchi kupata historia ya nchi yao kabla na baada ya uhuru.
Saturday, November 5, 2011
MAHAFALI YA 16 YA SEKONDARI YA AIRWING
Wednesday, November 2, 2011
JAJI CHIPETA AKITOA UFAFANUZI WA TCRA
POAC IKIWAJIBIKA KUYABANA MASHIRIKA YA UMMA
Subscribe to:
Posts (Atom)