Tuesday, September 11, 2012

NHIF YAPONGEZWA KWA HUDUMA NZURI

Keki iliyotolewa kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na Mjumbe wa Central Board of Education (CBE) Imran Dhalla ambaye ameridhishwa na huduma za NHIF.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Beatus Chijumba akipokea keki kutoka kwa Imran Dhalla ambaye ni Mwanachama  aliyeridhishwa na huduma za Mfuko.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Beatus Chijumba akimkabidhi keki hiyo Meneja Uanachama Binafsi,Grace Lobulu ambaye alimhudumia mwanachama huyo.

Ofisa Masoko na Elimu kwa Umma akimpa kipande cha keki mmoja wa wanachama aliyekuwepo wakati wa tukio hilo.

Meneja Masoko na Elimu Anjela Mziray na Ofisa wake Grace Michael wakiangali keki iliyoletwa na Mwanachama kwa lengo la kuushukuru Mfuko kwa huduma nzuri alizozipata.  

Kutokana na huduma nzuri zinazotolewa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), mmoja wa wanachama wa Mfuko huo, Imran Dhalla ambaye pia ni Mjumbe wa Central Board of Education (CBE) amefika katika Ofisi za Mfuko huo na kuupongeza kwa huduma nzuri na za haraka alizozipata.

Imran ambaye alikabidhi keki kwa Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Beatus Chijumba kama ishara ya kuridhishwa na huduma alizopata, alisema ushirikiano mkubwa alioupata ndio umemsukuma kuandaa keki hiyo na kufika ofisi za Mfuko huo kwa lengo la kuushukuru.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu Beatus Chijumba akipokea keki hiyo, alitoa mwito kwa wanachama kuupatia mfuko huo mrejesho wa huduma wanazopata ili uweze kuboresha zaidi.

"Mfuko uko tayari kupokea mrejesho wa aina yoyote, uwe mzuri au unaotutaka kuboresha zaidi...tunawaomba na wanachama wengine kuiga mfano huu ambao tunaamini utatusaidia sana kuboresha huduma zetu," alisema.

Imran alisema kuwa wafanyakazi wote wa mtandao wa shule za Al Muntazir wamejiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na mchakato unaendelea wa kuhakikisha wanafunzi nao wanajiunga na Mfuko huo ili wawe na uhakika wa matibabu.

No comments:

Post a Comment